• About Us
  • Blog No.1 Kwa Habari za Michezo na Burudani
  • Contact Us
  • Privacy Policy
Saturday, December 9, 2023
SOKALEO
  • HOME
  • KITAIFA
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI LEO
  • TETESI ZA USAJILI
No Result
View All Result
SOKALEO
  • HOME
  • KITAIFA
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI LEO
  • TETESI ZA USAJILI
No Result
View All Result
SOKALEO
No Result
View All Result

BAADA YA KUTOKA SARE NA AZAM JUZI…MABOSI YANGA WACHACHAMAA …ZAHERA ‘AMCHANA’ NABI UWEZO WA LOMALISA…

Chikao by Chikao
September 9, 2022
in KITAIFA
0 0
Share on FacebookShare on WhatsappShare on Telegram

 

YANGA imeangusha pointi mbili za kwanza katika Ligi Kuu Bara msimu huu baada ya sare ya 2-2 na Azam FC, japo imeendelea kushikilia rekodi ya kutopoteza mechi 40, lakini mabosi wao kuna kitu wamekishtukia katika kikosi hicho.

Mabosi wa Yanga wameshtukia kitu kama ambacho mashabiki wao wamekiona kwamba kuna shida katika safu yao ya ulinzi hasa baada ya kubadilishwa kwa kitasa wao Yannick Bangala kutoka kiungo hadi kuwa beki wa kati.

Awali msimu uliopita Bangala alicheza sambamba na kiungo Khalid Aucho katika kiungo mkabaji na kuleta utulivu kwa mabeki wao wa kati.

Tangu Bangala aanze kutumika kama beki wa kati Yanga imeyumba kwani katika mechi tatu za ligi imetoka salama mara moja pekee dhidi ya Coastal Union huku mechi nyingine zote ikiruhusu mabao ikiwa tayari imefungwa matatu, ikiwa na maana kila mechi imeruhusu bao moja.

Hatua hiyo imewaamsha mabosi wa Yanga na kuanza kufikiria upya kusaka beki wa kati wa maana ambaye atakuja kuongeza ugumu katika eneo la ulinzi.

Inafahamika kuwa  mabosi wa juu wa Yanga wamelijadili hilo masaa machache baada ya mchezo wa Azam.

“Tutatafuta beki wa haraka wa kati wako ambao tukiona wamepungua ubora tutaangalia uamuzi wa kuchukua lakini ni kweli safu yetu ya ulinzi imepungua makali,” alisema bosi huyo wa juu wa Yanga.

Mbali na kusaka beki huyo wa kati mabosi hao wamejipanga kuhakikisha wanaongea na makocha wao kumuulizia beki Ibrahim Bacca ambaye alionyesha uwezo bora katika mechi za mwisho msimu uliopita.

“Tuna yule Bacca hatutajua kwa nini bado anakosa nafasi tutazungumza na makocha na kama tukiona kama kuna haja ya kuzungumza naye kumjenga kiushindani tutafanya hivyo.

MSIKIE ZAHERA

Kocha Mwinyi Zahera aliyewahi kuifundisha Yanga alisema ameangalia mechi hiyo lakini akakazia lazima kazi ya kusaka mabeki wawili ifanyike.

Zahera ambaye yuko kwao DR Congo alisema ukiachana na beki wa kati pia upande wa kushoto nako kuna changamoto kama watacheza na timu yenye winga bora Yanga itapata shida.

“Nimeangalia hiyo mechi ilikuwa bora kiushindani, nadhani tumepata kipimo sahihi cha kujua ubora wetu, ligi ya hapo ilitakiwa kuwe na mechi kama hizo kama 10 zinasaidia kujua ubora wa timu yako,” alisema Zahera.

“Kule kushoto pia Lomalisa (Joyce) naye bado eneo lake timu pinzani zinapita sana akiwa anacheza yeye, nafikiri makocha wameyaona hayo na kuyafanyia kazi.”

Mchambuzi Ally Mayay, alisema Yanga inahitaji marekebisho katika nafasi ya ulinzi kabla ya klabu hiyo kwenda katika michuano ya kimataifa, hasa kwenye raundi ya kwanza.

“Angalia bao la pili dhidi ya Azam mabeki walikuwa wamesimama hivyo ni lazima wawe na nidhamu ya kukaba katika mashindano ya kimataifa timu pinzani zinatumia makosa hata kama dogo kwa kiasi gani,” alisema Mayay.

THIS POST IS POSTED IN SOKA LEO AND APPEAR IN THIS APP
ShareSendShare
Previous Post

KISA ‘MISHUTI YAKE YA MWANA UKOME’ FEI TOTO AIBUKA NA HILI YANGA….AFICHUA SIRI YA KUWATESA MAKIPA…

Next Post

BAADA YA KUONA ZORAN ALIVYOWAPELEKA PUTA SIMBA…AZAM FC WAAMUA KUMPA UKWELI HUU MAPEMA KOCHA WAO MPYA…

Related Posts

ihefu
KITAIFA

MASHUJAA MAMBO SIO MAMBO, HUKU IHEFU NAO WAFUFUKA KIMASIHARA

December 8, 2023
Ahmed Ally
KITAIFA

AHMED ALLY: NGOMA IKIWA NGUMU TUPATE ALAMA MOJA TU

December 8, 2023
lomalisa
KITAIFA

MAJEMBE YATAKAYOCHUKUA NAFASI YA MWAMBA LOMALISA

December 8, 2023
Simba chama
KITAIFA

MTEGO WA CHAMA DHIDI YA WYDAD UMEKAA HIVI

December 7, 2023
Load More

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Search Here

No Result
View All Result
ihefu

MASHUJAA MAMBO SIO MAMBO, HUKU IHEFU NAO WAFUFUKA KIMASIHARA

December 8, 2023
Ahmed Ally

AHMED ALLY: NGOMA IKIWA NGUMU TUPATE ALAMA MOJA TU

December 8, 2023
Pogba

POGBA KUKABILIANA NA KIFUNGO CHA MIAKA 4

December 8, 2023
lomalisa

MAJEMBE YATAKAYOCHUKUA NAFASI YA MWAMBA LOMALISA

December 8, 2023
Anza siku yako kimichezo kwakupitia ukurasa wa mbele wa gazeti la Mwanaspoti leo tarehe 8 December 2023, Pitia vichwa vya habari na ujipatie nakala yako leo.

TUNAANZIA HAPA!, GAMONDI MZUKA,MATAJIRI WASHTUA – MWANASPOTI LEO

December 8, 2023
Simba chama

MTEGO WA CHAMA DHIDI YA WYDAD UMEKAA HIVI

December 7, 2023

Msimamo wa Ligi Kuu

SOKALEO

© 2023 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

  • Home
  • Privacy Policy
  • Contact Us
  • About Us

No Result
View All Result
  • HOME
  • KITAIFA
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI LEO
  • TETESI ZA USAJILI

© 2023 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In