Mtandao mkubwa wa Time Media (وسائل الإعلام الوقت) kutoka nchini Misri imesifu ubora wa utangazaji wa Ligi kuu ya NBC na Azam TV, huku ikitolea mfano goli zuri lililofungwa na Stephane Aziz KI likitangazwa kupitia Azam TV Channels Network.
Mtandao huo mkubwa kutoka nchini Misri umesema utangazaji wa Ligi kuu ya Tanzania ni mzuri kuliko utangazaji wa Ligi kuu ya Misri ambao umekuwa mbaya zaidi msimu huu, wakitoa hongera kwa kampuni ya urushaji na utangazaji wa mechi ambayo ni Azam TV.
Time Media (وسائل الإعلام الوقت) imeandika kwamba, ukitazama goli nzuri la Stephane Aziz KI kwenye Ligi kuu Tanzania bara unaipa sifa nyingi na madhubuti kwa video za HD na utangazaji bora kutoka Azam TV Channels Network.
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YETU YA SOKALEO >>BONYEZA HAPA<<< KUIDOWNLOAD PLAYSTORE