Afisa Habari wa Yanga Ally Kamwe amezungumza leo na waandishi wa habari nakusema wamepata mwaliko wa mechi ya kirafiki nchini Malawi Julai 6, 2023 dhidi ya Big Bullets
“Tumepokea mwaliko maalumu kutoka kwa Serikali ya Malawi kucheza mchezo maalumu kwenye maadhimisho ya miaka 59 ya Uhuru wa Malawi itakayofanyika Julai 6, 2023. Ni heshima kubwa sana kwa Klabu yetu na kwa Taifa kwa ujumla”
“Siku ya maadhimisho tutacheza na Nyasa Big Bullets ya Malawi na Juai 5 tutakutana na Rais wa Malawi Lazarus Chakwera”
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YETU YA SOKALEO >>BONYEZA HAPA<<< KUIDOWNLOAD PLAYSTORE