Msanii wa BongoFleva, Rajabu Abdul Kahali ‘Konde Boy’ ama Harmonize amesema amewahi kupata kipigo kutoka kwa aliyekuwa mpenzi wake Kajala Masanja.
Harmonize ameandika mengi kwenye Insta Story kuhusu maneno ya Kajala wakati wa kipindi chake cha runinga ambayo Harmonize ameonesha kutofurahishwa nayo. Msanii huyo anyetamba na kibao chake cha ‘Single Again’ ametaka atajwe pia kwa mazuri aliyomfanyia X-wake huyo ikiwa ni pamoja na kulipa faini ya mzee wake Masanja ili asifungwe gerezani.
“Endeleeni na maisha yenu. Nisemeni sio tu kwa mabaya yangu hata mazuri. Msitegemee kukatazwa kutumia maudhui ‘content’ inayonihusu kikawaiada hata kisheria tumieni hadi mchoke.
“Ila mazuri msiyafumbie pia ili twende sawaa we had some good moments elezea basi. Sema natamani nione siku ukisema hapo kwenye tv about last moment how you ulivyonirushia matusi ukanipiga ili nikugeuzie ujipost nimekupiga and I was smart kifupi nilikushtukia and ndio maana ulihisi nakudharau!!!
“Ambia watu, mabwana wangapi wamekunyang’anya hadi simu natamani uwaambie ulivyokuwa unasumbua TRA kutaka kujua kama nimekupa card feki ya gari maskini Mungu huamini Frida Lol
“I have paid all mzee masanja ili asifungwe husemii subiri nilewe anyways good ndio ubinadamu ila reality ingenoga sanaa haya mnayoacha kuyasema.”
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YETU YA SOKALEO >>BONYEZA HAPA<<< KUIDOWNLOAD PLAYSTORE