Kocha Mkuu wa Simba, Robertinho. akizungumzia kutumia washambuliaji wawili kwenye mchezo mmoja ambao ni Phiri na Baleke alisema amegundua kitu kutoka kwao akiweka wazi kuwa akifanya hivyo ana uhakika wa kupata mfungaji bora kutoka katika nyota wake hao ambao amekiri kuwa kila mmoja anakuwa na kiu ya kufunga.
“Baleke na Phiri wote ni wachezaji wazuri kwenye umaliziaji na kila mmoja ana kiu ya kufunga hivyo naweza kutengeneza pacha nzuri na yenye faida kwa timu hasa kwenye suala la ushindani wa kupachika mabao mengi,” alisema Robertinho na kuongeza;
“Lakini wakati watatu hao wakifanya vizuri ameingia kati Kramo pia amekuwa mchezaji ambaye anajituma sana ameongeza chachu ya ushindani kwenye kikosi changu, nafurahia kuwa na wachezaji wenye malengo yanayofanana naamini sasa kila nitakayempa nafasi atanipa matokeo chanya.”
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YETU YA SOKALEO >>BONYEZA HAPA<<< KUIDOWNLOAD PLAYSTORE