Uongozi wa Namungo fc umethibitisha kutokea ajali iliyohusisha mashabiki wa timu hiyo waliokuwa wakisafiri kwenda Dar es salaam kushuhudia mchezo wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Yanga utakaopigwa leo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Namungo leo septemba 20, 2023 ajali hiyo imetokea eneo la Miteja karibu na Somanga, mkoani Lindi.
Aidha, ajali hiyo imesababisha vifo vya mashabiki wanne huku wengine 16 wakijeruhiwa.
Sokaleo.com tunatanguliza salamu za pole kwa klabu ya @namungofc Familia, Ndugu, Jamaa na Marafiki pamoja na wote walioguswa na msiba huu.
Bwana ametoa, Bwana ametwaa jinalake lihimidiwe.
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YETU YA SOKALEO >>BONYEZA HAPA<<< KUIDOWNLOAD PLAYSTORE