Golikipa wa Manchester United, Andre Onana amekiri kuwa kutokana na makosa aliyofanya akiwa golini yamesababisha kufungwa mabao 4-3 dhidi ya Bayern Munich mechi ya UEFA hatua ya makundi.
Onana ameyasema hayo katika mahojiano baada ya mechi akieleza; Baada ya kufanya kosa na kuruhusu bao tulipoteza hali ya mchezo, mimi ndiye nilisababisha, ni makosa yangu hakika,”
“Nawajibika kwa hili kwasababu hatujashinda na nachukulia kama fundisho kwasasa na baadae. Natakiwa kuboresha vitu vingi sana kwasababu mwanzo wangu hapa haujawa mzuri,” amesema Onana
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YETU YA SOKALEO >>BONYEZA HAPA<<< KUIDOWNLOAD PLAYSTORE