Mratibu wa Simba, Abbas Ally amefunguka akisema ni kweli walikuwa na mpango wa kwenda Kenya kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki na walipata mwaliko wa kucheza dhidi ya Police na Gor Mahia, lakini hawatafanya hivyo.
“Tulipata mechi mbili za kirafiki, lakini Chama cha Soka cha Kenya kimetuomba kucheza mechi hizo bila kuruhusu mashabiki kitu ambacho siyo rahisi kutokana na ukubwa wa timu yetu ambayo ina mashabiki wengi kila upande, hivyo tunahofia watajitokeza kwa wingi na sisi tukaonekana tumewadharau,”
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YETU YA SOKALEO >>BONYEZA HAPA<<< KUIDOWNLOAD PLAYSTORE
shafiikuntelela120@gmail.com