Rais Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa zawadi ya Sh 10 milioni kwa kila goli litakalofungwa katika mchezo wa African Football League kati ya Simba SC dhidi ya Al Ahly.
Mchezo huo wa ufunguzi utapigwa12:00 jioni dimba la Mkapa.
Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa ametoa taarifa hiyo alipozungumza na waandishi wa habari akiwa kata ya Mbagala, Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam, ambako Simba wanaendelea na hamasa kuelekea mchezo huo.
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YETU YA SOKALEO >>BONYEZA HAPA<<< KUIDOWNLOAD PLAYSTORE